Wednesday, June 12, 2013

Kundi La ORIJINO KOMEDI La Saini Mkataba Mkubwa Na Kampuni Ya NEXUS


Kundi la Orijino Komedi leo limakamilisha makubaliano ya mkataba wa usimamizi mpya wa kazi zao chini ya uongozi wa kampuni ya Nexus Consulting Agency na Rockstar 4000.
Msemaji wa Orijino komedi Sekione David  amesema Nexus  Consulting Agency imenunua haki zote za usimamizi wa biashara.Nexus itasimamia kipindi chao cha komedi na kuhakikisha kina fika mbali zaidi. Fahamu kuwa usimamizi huu utakuwa wa kazi za orijino komedi na kazi zingine za wasanii wa orijino komedi zinazo husu sanaa yao. Members wote wa Kundi hilo walikuwepo kwenye mkutano leo asubuhi pale Serena Hotel, Joti, Mac Regan, Masanja, Wakuvanga, Seki David, Mpoki na Vengu Ndani ya suti.
Pia kwa wale wa nje ya Tanzania soon Orijino komedi itaanza kuonekana nchi tofauti Afrik, kitu kilicho zua swali la je lugha wanayo tumia itabadilika, Well subtitles itahusika sana kwa zile nchi zisizo tumia lugha ya kiswahili. 
Source:Sam Misago

No comments:

Post a Comment