Saturday, July 20, 2013

PICHA:MAPOKEZI YA WANAJESHI WALIOUAWA HUKO DARFUR SUDAN.

 
Miili ya wanajeshi saba mashujaa wa Tanzania waliofariki wakiwa kazini wakitekeleza ulinzi wa amani wa kimataifa katika mkoa wa Darfur nchini Sudan, imewasili leo kwa ndege maalumu ya Umoja wa Mataifa.

Kaimu Mkurugenzi wa habari wa JWTZ, Meja Joseph Masanja amesema miili hiyo imewasili leo Jumamosi majira ya saa 9.45 alasiri katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa JNIA na imehifadhiwa katika hospitali ya jeshi ya Lugalo hadi Julai 22 ambapo itaagwa rasmi.

Miili iliyowasili ni ya Sajenti Shaibu Othuman, Koplo Oswald Chaula, Koplo Mohamed Juma, Koplo Mohamed Chikilizo, Pte. Rodney Ndunguru, Pte. Peter Werema na Pte. Fortunatus Msofe.

Shughuli za kuagwa miili ya wanajeshi hao zitafanyika katika viwanja vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga taifa vilivyoko Upanga jijini Dar es salaam.

Kuwapoteza wanajeshi hawa ni la kwanza na kubwa kwa nchi ya Tanzania tangu Tanzania ilipoanza kuchangia walinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa mwaka 2007. Wanajeshi wengine watatu wa Tanzania walifariki dunia mwezi uliopita baada ya chombo chao cha kusafiria kusombwa na maji ya mto uliokuwa umefurika huko nchini Sudan. 


Baadhi ya picha za mapokezi yao.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

PICHA:MHESHIMIWA AKIWA NA FAMILIA YAKE.

Mhe. Mwigulu Nchemba na familia yake

#PATRICK NGOWI|ENDORSED

 
 All the way from Arusha, Tanzania ,Patrick Ngowi Founder & C.E.O Of Helvetic solar
>>1st Place Winner of Top 100 Mid Sized Companies in Tanzania 2012-2013 
                    >> Forbes under 30 Best African Entrepreneurs 2013
                 >>With Only 28, Forbes list TWICE in 2013 Alone.
     >>Nominated for Young Person of the Year – The Africa Prize - The Nobel Prize for Young Africans-->Read More>>>
 Following its nomination by Tanzania’s leading consulting and auditing firm (KPMG) in 2012 as the fastest growing company in the country, Helvetic Solar and its founder, Patrick Ngowi have from then been featured in a number of national and international media including FORBES, Venture Africa, and most recently, he was invited to speak at the Africa Global Business Forum 2013 that was held in Dubai.
Follow Him On Twitter here-->https://twitter.com/PatrickNgowi



Friday, July 19, 2013

Africa’s Brightest & Best!| List 10 Nominees for The Future Awards Africa Young Person of the Year 2013|Patrick Ngowi All The Way From Arusha on The List.


The-Future-Awards-2013-New-600x406The Central Working Committee (CWC) of The Future Awards Africa has unveiled the list for the biggest youth award on the continent, the Young Person of the Year – The Africa Prize. The Future Awards Africa which has been described by the World Bank as ‘The Nobel Prize for Young Africans’, partners with the African Union (AU) this year.
As is the tradition, the nominees for Young Person of the Year – The Africa Prize, were drawn from a huge pool of talented trailblazers across Africa, who are making tremendous contributions around the globe,” said Dr. Raymonde Agossou, Head, Division for Human Capacity and Youth Development, African Union Commission. “We are extremely proud of our honorees this year. Working with The Future Project to compile this impressive list was refreshing.”
The winner of this award will be announced at the awards ceremony to hold in August 2013, in addition, all the honourees will be given plaques.

Ludwick Marishane – South Africa (22)
The Future Awards Young Person of the Year Honourees - BellaNaija - July2013 (1)
South Africa’s youngest patent holder and serial inventor, Ludwick Marishane is the founder of DryBath, the world’s only non-water based germicidal bath substitute lotion for the whole body which has sold 162 units as at 2012. He was rated as the best student entrepreneur in the world (Global Champion of the Global Student Entrepreneurs Awards 2011), one of the 12 winners of Google’s annual Zeitgeist Young Minds Competition, and appeared on Huffington Post and Ted Talks in 2012.
William Kamkwamba – Malawi (25)
The Future Awards Young Person of the Year Honourees - BellaNaija - July2013 (5)
A student in the Dartmouth College class of 2014, William Kamkwamba is a Malawian inventor and author who rose to global fame when he built a windmill to power some electrical appliances at their family house back at the age of 14. In 2012, Kamkwamba published his autobiography, an inspirational book, The Boy Who Harnessed the Wind: Creating Currents of Electricity and Hope and a documentary about Kamkwamba, called William and the Windmill, won the Documentary Feature Grand Jury award at SXSW in 2013.
Ashish J. Thakkar – Uganda (32)The Future Awards Young Person of the Year Honourees - BellaNaija - July2013 (6)
Ashish J. Thakkar is the Managing Director of Mara Group, a conglomerate he founded at the age of 15 which includes IT, real estate, manufacturing companies, and more with operations in 26 countries, spanning four continents, and employing over 7,000 people worldwide.
Saran Kaba Jones – Liberia (31)The Future Awards Young Person of the Year Honourees - BellaNaija - July2013 (1)
Saran Kaba Jones is a clean water advocate and social entrepreneur who founded FACE Africa to provide safe drinking water and empower women and girls in her home country of Liberia; FACE Africa had raised over $250,000 to this end and Jones was listed by the Guardian UK in 2013 as one of Africa’s 25 Top Women Achievers alongside President Joyce Banda of Malawi and Nobel Laureate Leymah Gbowee.
Moctar Dembele – Burkina Faso (22)The Future Awards Young Person of the Year Honourees - BellaNaija - July2013 (2)
Moctar Dembélé, one half of the team of African students that invented The Faso Soap, together with his partner, (Gérard Niyondiko, from Burundi), he is the first non-American born/citizen, to win the Global Science Venture Competition (GSVC) organized by the University of California Berkeley, USA for inventing the anti-malaria repellant soap.
Grace Ihejiamaizu – Nigeria (22)The Future Awards Young Person of the Year Honourees - BellaNaija - July2013 (2)
Named as one of Google’s 12 Brightest Young Minds in 2011, and by the US Government as ‘International Exchange Alumni Member of the Month for September 2012’, Grace Ihejiamaizu is an entrepreneur and global change-maker. In 2010, she founded an after-school youth project, Raising Young Productive Entrepreneurs (RYPE) Initiative; in 2012, she started a Social Enterprise company called iKapture Networks and founded the fast-growing online platform, opportunitydesk.org.
Patrick Ngowi – Tanzania (28)The Future Awards Young Person of the Year Honourees - BellaNaija - July2013 (3)
Following its nomination by Tanzania’s leading consulting and auditing firm (KPMG) in 2012 as the fastest growing company in the country, Helvetic Solar and its founder, Patrick Ngowi have from then been featured in a number of national and international media including FORBES, Venture Africa, and most recently, he was invited to speak at the Africa Global Business Forum 2013 that was held in Dubai.
Peter Okoye and Paul Okoye (PSQUARE) – Nigera(31)The Future Awards Young Person of the Year Honourees - BellaNaija - July2013 (4)
This inspiring twin brothers have been tagged one of the very best in African music. Signed to Akon’s Konvict Musik, Psquare signed a record distribution deal with Universal Music Group in 2012, the same year they released their hugely successful remix singles/videos featuring global music giants, Akon “Chop My Money”, and Rick Ross “Beautiful Onyinye Remix”. The duo has just come off a massively successful African tour where they easily filled up stadia in Malawi, South Africa, Uganda, Zimbabwe, Equatorial Guinea, Congo Brazzaville, and more.
Fohlabenchi Lily Haritu – CAMEROON (27)The Future Awards Young Person of the Year Honourees - BellaNaija - July2013 (7)
A finalist of the 2013 Commonwealth Youth Awards for Excellence in Development Work, Foglabenchi Lily Haritu, is the youngest individual to reach the position of program supervisor in the Cameroon Baptist Convention Health Services. Haritu has demonstrated an outstanding commitment to reproductive and sexual health rights education and rights promotion particularly through her work with stationary and rural mobile clinics across Cameroon.
Kariuki Gathitu – Kenya (27)The Future Awards Young Person of the Year Honourees - BellaNaija - July2013 (1)
Kariuki Gathitu is an entrepreneur, and software developer who in 2010 turned down an offer to work for Google to instead developed a mobile payment management system called MPAYER. MPAYER has been widely acknowledged and received awards for innovation and recently won second position in a global competition held in South Africa called Dragons Den (2013) and was the best application in Africa; it came second in the World’s 50 Top Startups Globally (2013), and in same year was named one of the Top Tech Start ups You Need to Know in Africa by CNN.

NAMBA ZA SIMU ZA MAWAZIRI ILI KUWATUMIA MAONI KUHUSU KODI YA SIMU


Kufuatia kauli za Serikali magazetini kuhusu mimi na kodi ya umiliki wa kadi za simu; nijibu tu kwa ujumla kwamba SITAACHA. Badala yake naomba kuwapatia namba zao: Makamba 0767783996 na Mgimwa 0754/0684765644, tunachohitaji ni kauli ya Serikali kuwa kodi imesitishwa na itaondolewa na sio siasa chafu.

Kwa mliotaka msimamo wangu juu ya kauli ilinukuliwa jana tarehe 18 Julai 2013 na Gazeti la Majira kwamba Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Januari Makamba kwamba; “Mnyika anaangalia upepo unakoelekea, akiona watu wanalalamika ndipo anaongea namsihi aache kufanya siasa katika jambo hili”, naomba kutumia mtandao huu kutoa majibu ya ujumla kwa maswali na masuala yote kama ifuatavyo:

Nieleze kwamba sitaacha kufanya siasa kwenye jambo hili mpaka kodi hiyo itakapofutwa kuwawezesha wananchi wa kipato cha chini kubaki na fedha walau kidogo kwa maendeleo.

Sitaacha kufanya siasa kwa sababu ndio kazi yangu ambayo wananchi walinichagua kuifanya ya kuwawakilisha na kuisimamia Serikali ambayo yeye Makamba ni sehemu yake. Sitaacha kufanya siasa kwa sababu Mwalimu Nyerere alisema ili nchi yetu iendelee inahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora.

Ambacho sitafanya ni siasa chafu kama hizo ambazo Makamba amefanya za kusema uongo, kwa kuwa naamini anafahamu kabisa kwamba sijaanza kuongea kuhusu suala hili baada ya malalamiko ya wananchi bali jambo hili nilianza kulishughulikia bungeni mara baada ya Waziri wa Fedha kuwasilisha jedwali la marekebisho la kuanzisha kodi lukuki za simu ikiwemo hii. Katika mchango wangu bungeni, nieleza kwamba muswada huo wa sheria ya fedha kwa kupandisha kodi kwenye mafuta na simu ni ‘muswada wa majanga ya kuwaongezea mzigo wa gharama za maisha kwa wananchi.

Aidha, sikuishia kusema tu kwa niaba ya wananchi bali nilichukua hatua kwa mujibu wa kanuni za Bunge nami kuwasilisha jedwali la marekebisho ya kupinga kodi ya umiliki wa kadi za simu pamoja na kodi nyingine zote zenye kuongeza mzigo wa gharama za maisha kwa wananchi sio kwenye sekta ya mawasiliano bali pia kwenye sekta zingine ikiwemo sekta ndogo (sub sector) nyeti ya mafuta.

Mlioniuliza kwa SMS katika simu na kwenye mitandao ya kijamii sasa ni wakati wa Makamba kuhojiwa kwa njia hizo hizo (Simu yake ya Mkononi ni 0767783996) kwa kuwa yeye ni sehemu ya Serikali na Serikali ndiyo ambayo iliingiza suala hili kwa mara ya kwanza ndani ya ukumbi wa Bunge kupitia hotuba ya Bajeti Serikali na ikalirudia kuliingiza kupitia jedwali la marekebisho ya Sheria ya Serikali; ni wakina nani hasa kwa majina ndani ya Serikali na Bunge walioingiza kodi hii? Na ni wakina nani hasa waliopigia kura ya ndio kuipitisha?

Aidha, amenukuliwa na gazeti la Mwananchi la leo tarehe 19 Julai 2013 akieleza kwamba hakubaliani na suala hili na kupita kwake ilikuwa na kuzidiwa nguvu. Hivyo, ataje kwa majina hayo waliozidi nguvu serikali kinyume na matakwa yake. Amenukuliwa akisema pia kwamba anajua kuwa suala hili haliwezi kutekelezwa na kwamba ni lazima litabadilishwa kwa kuangalia eneo lingine la kutoza kodi. Ni vizuri akahojiwa, ikiwa huo ni msimamo wa Serikali; mwenye mamlaka ya kusitisha kodi hiyo ni nani na kwanini hajitokezi kutoa agizo la kusitisha wakati maandalizi yakiendelea ya kupeleka muswada bungeni wa kuifuta kabisa kodi hiyo katika mkutano ujao?

Wakati Naibu Waziri akisema hayo, Waziri wa Fedha Dk William Mgimwa katika Serikali hiyo hiyo yeye ametoa kauli tofauti siku hii hii ya leo ambapo kwa mujibu wa gazeti la Mtanzania amewataka watumiaji wa mitandao ya simu nchini na watanzania kwa ujumla kuwa na subira kuhusu tozo ya sh 1000 kwa mwezi kwa kila laini ya simu za kiganjani.

Na kwa kuwa amesema kwamba Serikali inaendelea kupokea maoni kutoka kwa wadau, natoa mwito kwa wananchi kumtumia maoni kupitia namba zake za simu za mkononi 0754/0684-765644. Aidha, ni vizuri aeleze subira hiyo ivutwe mpaka lini? Na ni wakina nani hasa kwa majina waliomfanya akaingiza kodi hiyo katika kitabu cha Hotuba yake aliyosoma bungeni kuhusu bajeti ya Serikali na wakina na hasa kwa majina waliomfanya arejeshe kodi hiyo ya kadi za simu kwenye jedwali la marekebisho ya muswada wa sheria ya fedha alilowasilisha bungeni.

Nasisiza kuwa kauli za ujumla za Serikali bila kuwataja kwa majina wahusika ni za kujivua mzigo wa lawama baada ya malalamiko ya wananchi kuhusu kodi hii na nyinginezo kwa kuhamisha mzigo huo kwa wabunge. Ni muhimu badala ya kutoa kauli za ujumla za kulaumu wabunge, Rais ama kiongozi mwingine mwenye mamlaka ajitokeze kusitisha kutozwa kwa kodi hiyo na kuanzisha mchakato wa muswada wa kufuta kodi hiyo kuwasilishwa katika mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanza tarehe 27 Agosti 2013.

Majina ya wahusika yasipotajwa au mamlaka zinazohusika zisipotoa kauli katika mkutano wa hadhara nitakaoshiriki jumapili tarehe 21 Julai 2013 katika Uwanja wa Sahara kata ya Mabibo kuanzia saa 8 Mchana mpaka saa 11 Jioni nitatoa mrejesho kuhusu yaliyojiri katika mkutano uliopita wa Bunge na kueleza hatua zaidi zinazopaswa kuchukuliwa kuwezesha majina ya wabunge hao kutajwa hadharani na hatua za kuondoa kodi hiyo kuchukuliwa. 



Uongozi bora na uraia mwema wenye uwajibikaji ni chimbuko na chachu ya ukuaji endelevu wa uchumi wa nchi na ustawi wa maisha ya wananchi. Twende kazi.
John Mnyika (Mb)
19 Julai 2013

FAHAMU:10 BEST ALBUMS WIKI HII


1] Jay Z - Magna Carta... Holy Grail

2] Ciara – Ciara


3] J Cole - Born Sinner 
 
4] Florida Georgia Line - Here's To The Good Times


5] Imagien Dragons - Night Visions 
 

6] Kanye West - Yeezus


7] Wale - The Gifted


8] Skylar Gray - Don't Look Down 
 

9] Daft Punk - Random Access Memories 

10] Macklemore & Ryan Lewis - The Heist 

WEMA SEPETU APANDISHWA KIZIMBANI KWA MARA YA KWANZA BAADA YA KUMTUKANA MENEJA WA HOTELI

KUNA kila dalili kwamba mrembo anayetamba kwenye filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu   jela inamwita na anatakiwa kufanya maombi ili kukwepa kifungo maishani mwake.

Hali hiyo inafuatia staa huyo kupandishwa kizimbani kwa mara nyingine tena Jumatano iliyopita, pale alipopanda katika Mahakama ya Mwanzo ya Kawe jijini Dar kwa kosa la kumpiga na kumtukana matusi ya nguoni meneja wa hoteli moja iliyopo Kawe Beach jijini Dar, Godluck Kayumbu.


Kabla ya  kupandishwa  kwa ‘pilato’,  staa huyo anayemiliki Kampuni ya Endless Fame alikuwa akisakwa na askari kwa siku kadhaa na kufanikiwa kuwapiga chenga za hapa na pale.
 

Hata hivyo, mbio zake ziliishia ukingoni Julai 16, mwaka huu, alipokamatwa saa mbili usiku akiwa anafuturu na wageni wake nyumbani kwake, Kijitonyama Dar. 


Askari saba walifika nyumbani kwake wakiwa ndani ya Land Rover ‘difenda’ kwa ajili ya kumkamata, hata hivyo walipata upinzani kidogo kutoka kwa mlinzi wa staa huyo ambaye alikuwa akizuia bosi wake asikamatwe ambapo ilibidi askari hao wakaze msuli na kutuliza mtiti uliokuwa ukitaka kutokea.
 
 Baada askari kumfikia staa huyo, walimtaka kwenda naye kituo cha polisi kwa kutumia difenda walilofika nalo ambapo Wema alipinga na kugeuka mbogo kwa kudai kwamba hawezi kupanda difenda kutokana na hadhi yake.

Pamoja na askari kutaka kumpandisha kwa nguvu, staa huyo alipinga na ikakubaliwa apande gari lake aina ya Audi Q7 huku akiwa chini ya ulinzi wa askari.

Safari ikaishia Kituo cha Polisi cha Kawe ambako staa huyo aliandikisha maelezo na baada ya zoezi hilo akatupwa selo. 


Kama lilivyo jina lake, wema hauozi, staa huyo alipata dhamana saa 5 za usiku baada ya kudhaminiwa na msanii  mwenzake wa filamu, Kajala Masanja.

Kajala aliwahi kutolewa katika mdomo wa jela na Wema siku za nyuma baada ya kukutwa na hatia na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar alipotakiwa kulipa faini ya shilingi milioni 13 au kwenda jela, Wema alimlipia kiasi hicho cha fedha. 

Wapambe wa Wema waliokuwa wamejazana nje ya kituo hicho cha polisi, walilipuka kwa shangwe baada ya bosi wao kuchomolewa kutoka selo. Staa huyo aliondoka na gari lake lililokuwa likiendeshwa na meneja wa kampuni yake aitwaye Petit Man.
Julai 17, asubuhi Wema alirudi kituoni hapo na kuwekwa chini ya ulinzi kwa ajili ya kupelekwa mahakamani kusomewa mashitaka yake.

 Katika hatua ya kushangaza, staa huyo alitembezwa kwa miguu umbali wa mita 200 kutoka kituo cha polisi hadi Mahakama ya Mwanzo ya Kawe.  


Wema alipandishwa kizimbani na kusomewa mashitaka yake na Mh. Hakimu, Bernice Ikanda na kudaiwa kufanya vurugu, kushambulia kwa kumpiga makofi na kumtukana Kayumbu.
Mbele ya hakimu, Wema alikana mashitaka na hakimu aliiahirisha kesi hiyo mpaka Julai 31, mwaka huu.

FAHAMU:Eminem Kukataa Kuigiza Kwenye Filamu Ya Elysium. Fahamu Nani Kachukua Nafasi Yake.

 
Awali Ilisemekana kuwa star Eminem amepigwa chini kwenye orodha ya stars waliochaguliwa kuigiza kwenye filamu mpya ya "Elysium".Bonyeza Read More kufahamu Zaidi
Sasa chukua hii, Ukweli ni kwamba Rapper/ Actor Eminem alikata kuigiza kwenye filamu hio baada ya watayarishaji kumwambia kuwa mji wake wa Detroit haupo kwenye orodha ya sehemu itakayo fanya hio filamu.
Eminem anafahamika kuwa mstari wa mbele katika kuonyesha mapenza na mji wake wa Detroit huko Michigan na mapenzi hayo yamesababisha akose nafasi ya kuwa Main Character wa Filamu ya Elysium. Sehemu hio amepewa mwigizaji Matt Damon aliye kuwa mtu wa tatu kwenye orodha ya watu wanaoweza kuicheza hio sehemu vizuri kwa mujibu wa Director wa filamu hio Neil Blomkamp's.

Kwa mujibu wa Rolling Stone, Mtu wa kwanza kupewa mchongo huo alikuwa rapper kutoka South Africa Ninja.
  
 Elysium Ipo theaters August 9.  
Credit:Sam Misago

FAHAMU:CHADEMA YAJITOA KUWANIA UMEYA WA ARUSHA


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeamua kuachana na kuwania umeya wa Jiji na badala yake kimemwomba Meya, Gaudence Lyimo (CCM), atende haki.

Katibu wa Kanda ya Kaskazini wa chama hicho, Amani  Golugwa alisema jana, kwamba Chadema haina uroho wa madaraka kama baadhi ya watu wanavyofikiri, bali inasimamia vipaumbele vya maendeleo.


Hata hivyo, kauli hiyo inapingana na nyingine ya chama hicho ya wiki hii pia, kwamba ushindi katika uchaguzi mdogo wa kata nne, ni chachu katika msimamo wa chama kutaka uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha, urudiwe.

Mwenyekiti wa Madiwani wa Chadema, Isaya Doita, ndiye aliyenukuliwa wiki hii akisema hayo, akiamini kuwa Meya Lyimo wa CCM, alichaguliwa kimizengwe.

Baada ya Chadema kutetea viti vyake vinne vya udiwani kwenye uchaguzi mdogo wa hivi karibuni, kimefikisha viti 15 kwenye Baraza la Madiwani la Arusha, huku CCM ikibaki na viti 12 na TLP sita.
 

Pia Chadema ina nafasi ya kuongeza kiti, kwani ina nafasi moja ya viti maalumu iliyokuwa inakaliwa na Rehema Mohamed, aliyetimuliwa mwaka 2011.

Hata hivyo, pamoja na Chadema kuongoza kwa kuwa na viti vingi vya udiwani jijini hapa, haina uwezo wa kuweka Meya, bila kushirikiana na CCM au TLP.

Chadema ikikosa ushirikiano huo, ushirikiano wa CCM na TLP, utabaki kuwa na nguvu ya kuweka Meya na naibu wake madarakani, huku Chadema ikibaki kuwa kambi ya upinzani yenye nguvu katika Baraza la Madiwani.

Golugwa alisema Chadema haina uroho wa madaraka, bali inataka uchaguzi wa Meya wa Jiji urudiwe ingawa haitaki nafasi hiyo kwa kuwa si kipaumbele chake.
 

"Tunaangalia wananchi wanafikiwaje na maendeleo tuna imani muda si mrefu Jiji la Arusha litapata Meya ambaye amechaguliwa kwa misingi ya sheria," alisema Golugwa.  
 

"Hatuna shida na Meya wala hatuna uroho wa madaraka tunachopinga ni upatikanaji wa Meya huyo na tunamtaka afanye kazi zake kwa kusimamia misingi ya sheria na si upendeleo, tunahitaji kuona kila mwananchi ananufaika na maendeleo hadi mitaani," aliongeza.

Pia alikaririwa wakati mmoja akisema ushindi huo unaihakikishia Chadema wingi wa wajumbe katika Baraza  la Madiwani, hivyo kuwa na fursa ya kumwondoa Lyimo madarakani.

Thursday, July 18, 2013

INSTAGRAM||DIAMOND "AWAPA MAKAVU" HATERS



Inaonekana Diamond amechoshwa na haters wanaosubiri aanguke kimuziki na kumcheka...


Kupitia mtandao wa Instagram, Diamond ameamua kutupia picha inayomuonyesha akianguka kutoka juu (angani) na kufikia chini kwa kichwa kwenye barabara ya lami. 


Picha hiyo ilisindikizwa  na maelezo yanayosema , "Najua hiki ndio mnachokisubiri, kwahiyo endeleeni kusubiri"...# Haters
 

NEW VIDEO:LIL WAYNE - "GOD BLESS AMERIKA"

 http://api.ning.com/files/wrxP0oBpcejnll9Efp63QSaE*ZVU9ZFMfaFdZjieLHT8N9c4m6tAnD8vzrLbUPmKnunThPbtf7EPaKf*1mHZuJtzqzO4iHR9/weezy.png
Lil Wayne ameachia video mpya ya wimbo wake unaoitwa “God Bless Amerika” Video hiyo imeongozwa (Directed) na Eif Rivera na ilishutiwa katika mji wa nyumbani Hollygrove New Orleans, kule kitaani wanapoishi watu wa chini wenye maisha ya kawaida. Kwa sasa Wayne yuko kwenye tour yake inayoitwa America’s Most Wanted akiwa na T.I, 2 Chainz na wengine wageni waalikwa. Leo usiku watakuwa Pittsburgh. “God Bless America” imetoka kwenye album ya Weezy inayoitwa “ I Am Not Human Being II”…check video hapo chini…

MTV Music VIDEO AWARDS|FULL NOMINEES LIST



  Msimu mwingine wa MTV Video Music Awards na mwaka huu inaenda huko Brooklyn sehemu anayotokea Jay – Z nah ii ni kwa mara ya kwanza. Itakuwa tarehe 25 Agosti na watu mashuhuri wanaofanya muziki kutoka duniani watatokea kwenye stage hiyo hiyo ni HOV built Barclays Center. Check list nzima ya vipengele na washiriki.
                                                            Video of the Year
                                                     Justin Timberlake – “Mirrors”
                                         Macklemore & Ryan Lewis feat. Wanz – “Thrift Shop”
                                               Bruno Mars – “Locked Out of Heaven”
                                        Robin Thicke feat. T.I. and Pharrell – “Blurred Lines”
                                            Taylor Swift – “I Knew You Were Trouble”

Best Hip Hop Video
Macklemore & Ryan Lewis feat. Ray Dalton – “Can’t Hold Us”
Drake – “Started From The Bottom”
Kendrick Lamar – “Swimming Pools”
A$AP Rocky feat. Drake, 2 Chainz and Kendrick Lamar – “F–kin’ Problems”
J. Cole feat. Miguel – “Power Trip”

Best Male Video
Justin Timberlake – “Mirrors”
Robin Thicke feat. T.I. and Pharrell – “Blurred Lines”
Bruno Mars – “Locked Out of Heaven”
Ed Sheeran – “Lego House”
Kendrick Lamar – “Swimming Pools”

Best Female Video
Rihanna feat. Mikky Ekko – “Stay”
Taylor Swift – “I Knew You Were Trouble”
Miley Cyrus – “We Can’t Stop”
Pink feat. Nate Ruess – “Just Give Me A Reason”
Demi Lovato – “Heart Attack”

Best Pop Video
Bruno Mars – “Locked Out of Heaven”
Justin Timberlake – “Mirrors”
Fun. – “Carry On”
Miley Cyrus – “We Can’t Stop”
Selena Gomez – “Come and Get It”

Artist To Watch (Formerly Best New Artist)
Twenty One Pilots – “Holding On To You”
Zedd feat. Foxes – “Clarity”
Austin Mahone – “What About Love”
The Weeknd – “Wicked Games”
Iggy Azalea – “Work”

Best Collaboration
Justin Timberlake, feat. Jay-Z – “Suit & Tie”
Pitbull feat. Christina Aguilera – “Feel This Moment”
Calvin Harris feat. Ellie Goulding – “I Need Your Love”
Robin Thicke feat. T.I. and Pharrell – “Blurred Lines”
Pink feat. Nate Ruess – “Just Give Me A Reason”

Best Video With A Social Message
Kelly Clarkson – “People Like Us”
Macklemore & Ryan Lewis – “Same Love”
Snoop Lion – “No Guns Allowed”
Miguel – “Candles in the Sun”
Beyoncé- “I Was Here”

Best Rock Video
Imagine Dragons – “Radioactive”
Fall Out Boy – “My Songs Know What You Did in the Dark (Light Em Up)”
Mumford & Sons – “I Will Wait”
Thirty Seconds To Mars – “Up in the Air”
Vampire Weekend – “Diane Young”

Best Art Direction
Capital Cities – “Safe and Sound”
Thirty Seconds To Mars – “Up in the Air”
Janelle Monae feat. Erykah Badu – “Q.U.E.E.N”
Lana Del Rey – “National Anthem”
Alt-J – “Tesselate”

Best Choreography
Chris Brown – “Fine China”
Ciara – “Body Party”
Jennifer Lopez feat. Pitbull – “Live It Up”
will.i.am feat. Justin Bieber – “#thatPOWER”
Bruno Mars – “Treasure”

Best Cinematography
Thirty Seconds To Mars – “Up in the Air”
Lana Del Rey – “Ride”
Yeah Yeah Yeahs – “Sacrilege”
Macklemore & Ryan Lewis feat. Ray Dalton – “Can’t Hold Us”
A-Trak & Tommy Trash – “Tuna Melt”

Best Direction
Justin Timberlake feat. Jay-Z – “Suit & Tie”
Macklemore & Ryan Lewis feat. Ray Dalton – “Can’t Hold Us”
Yeah Yeah Yeahs – “Sacrilege”
Fun. – “Carry On”
Drake – “Started From The Bottom”

Best Editing
Pink feat. Nate Ruess – “Just Give Me A Reason”
Calvin Harris feat. Florence Welch – “Sweet Nothing”
Macklemore & Ryan Lewis feat. Ray Dalton – “Can’t Hold Us”
Justin Timberlake – “Mirrors”
Miley Cyrus – “We Can’t Stop”

Best Visual Effects
Capital Cities – “Safe and Sound”
Duck Sauce – “It’s You”
Flying Lotus – “Tony Tortures”
Skrillex feat. the Doors – ”Breakn’ a Sweat”
The Weeknd – “Wicked Games”

NEW MUSIC:M2TheP Ft CHEGGE & COUNTRY BOY - MASAMBEWENA

RAIS KIKWETE AMTAKA RAIS WA SUDAN AWASAKE WATU WALIOHUSIKA NA MAUAJI YA WANAJESHI WA TANZANIA HARAKA IWEZEKANAVYO


Rais Jakaya Kikwete amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na Rais wa Sudan, Omar Bashir, kuhusu kuuawa na kujeruhiwa kwa askari wa Tanzania, walioko katika ulinzi wa kimataifa wa amani katika jimbo la Darfur.

Taarifa ya Ikulu iliyotumwa kwa vyombo vya habari jana, imeeleza kuwa katika mazungumzo hayo, Rais  Kikwete alimtaka Rais Bashir kuchukua hatua za haraka kuwasaka na kuwakamata waliohusika na kitendo hicho kiovu, na kuwafikisha mbele ya sheria haraka iwezekanavyo.

Rais Bashir amekubaliana na Rais Kikwete na kumuahidi kuwasaka hadi kuwakamata wale wote waliohusika na kuwachukulia hatua za kisheria.

Alimueleza Rais Kikwete kuwa binafsi anaamini waliohusika ni wahalifu, kusisitiza kuwa lazima watasakwa hadi kukamatwa na kuchukuliwa hatua.

Alimpa pole Rais Kikwete kwa tukio hilo la kusikitisha, ambapo wanajeshi wa Tanzania walienda nchini Sudan kulinda amani na usalama wa wananchi wa Sudan.

Awali Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon, alimpigia Rais Kikwete na kumpa pole kwa mkasa huo mkubwa na wa kusikitisha, ambao umewatokea Watanzania hao wakati wakitekeleza jukumu lao la kulinda amani nchini Sudan.

Hadi sasa hakuna kikundi chochote kilichokiri kuhusika na shambulio hilo, ingawa kumekuwa na hali ya kutupiana lawama baina ya vikundi vya kiserikali na vya waasi katika jimbo la Darfur.

Mapigano baina ya vikundi vya kikabila na koo mbalimbali, yamesababisha mapigano na uvunjifu mkubwa wa amani na usalama katika jimbo la Darfur kwa muda wa miaka 10 sasa.

Mara nyingi mapigano na tofauti zao hizo zimesababisha vifo na uvunjifu wa amani kwa wananchi wa Sudan na wageni pia.

Mwishoni mwa mwaka jana wanajeshi wanne kutoka Nigeria, waliuawa karibu na El Geneina, Magharibi mwa Darfur, ambapo pia inaelezwa na AU kuwa wanajeshi wapatao 50, wameuawa tangu kikosi hicho cha Umoja wa Afrika kinachoundwa kwa chini ya Umoja wa Mataifa (UNAMID), kianze operesheni yake mwishoni mwa 2007.
 

Taarifa za UN pia zinaeleza kuwa kabla ya mashambulizi yaliyofanyika dhidi ya kikosi cha Tanzania Jumamosi iliyopita, wanajeshi sita wanaolinda amani waliuawa tangu Oktoba mwaka huu, ambapo pia inasadikiwa kuwa watu wapatao 300,000 wameyakimbia makazi yao.
Hata hivyo, kiini cha mgogoro huo inasadikiwa kuwa ni ugomvi wa ardhi na rasilimali zilizoko katika jimbo hilo nchini Sudan.

Miili ya maaskari hao saba wa Tanzania, inatarajiwa kuwasili nchini Ijumaa, Julai 19 kwa ajili ya maziko.
Credit:Gumzo La Jiji

HAPPY 95th BIRTHDAY NELSON MANDELA (MADIBA)

 




Afrika Kusini leo wanasherehekea miaka 95 ya kuzaliwa kwa Mzee Nelson Mandela huku rais huyo wa zamani bado yuko mahututi hospitalini.
Ilikuwa ikitabiriwa kwamba shujaa huyo wa vita dhidi ya ubaguzi wa rangi kwamba angeruhusiwa kwenda kusherehekea siku yake ya kuzaliwa lakini bado yuko hospitali kutokana na kurejea maambukizi kwenye mapafu.


Kituo cha Kumbukumbu ya Nelson Mandela na makundi mengine yamewataka watu kujitolea kwa dakika 67 kwa kazi za hisani kukumbukia miaka 67 ambayo Mandela aliitumikia jamii yake.

Umoja wa Mataifa pia umetambua mapambano ya Mandela dhidi ya ubaguzi wa rangi na kusema siku yake ya kuzaliwa ni fursa ya kuenzi urithi wake, na shughuli mbalimbali zimeandaliwa duniani kote.

Siku ya kuzaliwa Mandela, Julai 18, ilitangazwa rasmi kuwa Siku ya Kimataifa ya Mandela na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2009 kama kutambua mchango wake kwa utamaduni wa amani na uhuru.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon alisema Siku ya kuzaliwa Mandela mwaka huu imekuja katika wakati wa 'kuakisi kwa kina maisha yake na kazi ya Madiba, huku kiongozi huyo wa aina yake akiwa bado yuko hospitalini'
Aliongeza: "Nelson Mandela alijitolea miaka 67 ya maisha yake kupigania haki za binadamu na haki kwa wote."


Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma ataadhimisha siku ya kuzaliwa Mandela kwa kutoa michango ya nyumba kwa familia masikini katika eneo la Pretoria.

Mandela alilazwa hospitali mjini Pretoria Juni 8 kwa matatizo ya maambukizi kwenye mapafu yake.

Mapema wiki hii, Rais mstaafu Thabo Mbeki alibashiri kwamba Mandela anaweza kuruhusiwa kutoka hospitali mapema na kwenda kupatia nafuu nyumbani.

Marafiki ambao walimtembelea wamesema yuko kwenye mashine ya kusaidia maisha kwa ajili ya kusaidia tu kupumua kwa urahisi.
 

Taarifa rasmi za hivi karibuni kabisa kuhusiana na afya yake zilisema Mandela alikuwa kwenye hali mbaya lakini inayoimarika.

Lakini wote, mke wa Mandela, Graca Machel, na Rais Jacob Zuma wamesema hivi karibuni kwamba Mandela anaendelea vema na matibabu.

Shujaa huyo wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi alitumikia miaka 27 gerezani kabla ya kuja kuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini mwaka 1994