Saturday, June 8, 2013

HII NDO KAULI YA RAMA DEE KWA CLOUDS Fm BAADA YA KUSHINDA TUNZO

KALA JEREMIAH NA OMMMY DIMPOZ WAONGOZA KWA KUJINYAKULIA TUZO TATU TATU KILA MMOJA

Mwaka huu umekuwa mwaka mzuri zaidi kimuziki kwa msanii toka rock City Mwanza Kala Jeremiaha ambae maombi yake kwa ‘Dear God’ yamesikika na amepata majibu kwa njia ya kipekee na wimbo wake ‘Dear God’ umeweza kuchukua tuzo tatu katika Kilimanjaro Music Awards 2013.  
 
Kala Jeremiah ametumia mkuki mmoja kunasa ‘swala’ wake watatu muhimu mwaka huu, Dear God imeweza kumpa nafasi kubwa na kushinda tuzo katika kipengele cha wimbo bora wa Hip Hop.


Nguvu ya wimbo huo hapana shaka ndiyo imemuwezesha pia kuondoka na tuzo ya msanii bora wa Hip Hop na Mtunzi bora wa mashairi ya Hip Hop.

Kala aliweza kuwapenya wasanii wazito kama Fid Q, Joh Makini, Mwana FA, Profesa Jay na mdogo wake katika game Stamina wa Moro Town waliokutana nae katika vipengele vya Hip Hop.

Wimbo huu ulitengenezwa na mtayarishaji chipukizi Dee Classic ambae pia alikuwa anawania tuzo katika kipengele cha mtayarishaji chipukizi wa Mwaka lakini hakuweza kushinda tuzo hiyo ambayo ilienda kwa Mesen Selector.

Embedded image permalink
Msanii mwingine wa bongo fleva aliyeng’ara katika tuzo hizo ni Ommy Dimpoz ambae pia aliondoka na Tuzo tatu, ambazo ni Video bora ya wimbo bora ya mwaka, wimbo bora wa Bongo Pop ‘Me and You’ akiwa na Vannessa Mdee ambao pia uliwapa tuzo ya wimbo bora wa kushirikishwa/kushirikiana.

Wasanii na watayarishaji wa muziki wa bongo fleva ambao kwa mara ya kwanza wameweza kujishindia tuzo za Kili ni pamoja na kundi la Jambo Squared toka Arusha (Kundi bora la muziki wa kizazi kipya), Rama Dee ‘Kinega’ (Wimbo bora wa RnB ‘Kuwa na subira).

Wengine ni Amini (Wimbo bora wa Zouk Rhumba ‘Ni wewe’), Recho (Msanii bora wa kike Bongo fleva), na Nay wa Mitego (Wimbo bora wa Hip Hop ‘Nasema Nao’). Mesen Selecter (Mtayarishaji chipukizi wa Mwaka), Ali Nipishe (Msanii bora anaechipukia).

Tuzo hizo zimeshuhudiwa huku mfalme na malkia wa muziki wa kibongo wakitangazwa kuwa Lady Jay Dee ‘Anaconda’ (Msanii bora wa Kike) na Diamond Platinumz (Msanii bora wa kiume).

MTOTO WA KITANZANIA WA MIAKA 14 ANAYETENGENEZA APLICATION ZA SIMU NA KUWAUZIA NOKIA

Mtoto Alvin akisalimiana na Rais wa
Tanzania Mh.Jakaya Kikwete
Alvin Walter Makundi ni kijana mdogo wa Kitanzania
 anayeishi na wazazi wake nchini Singapore. 
Akiwa na umri wa miaka 14 na mwanafunzi wa
 kidato cha pili huko Singapore, tayari
 ameshatumbukiza jina lake katika orodha ya
 wataalamu wa application katika moja ya makampuni
 makubwa duniani ya kutengeneza simu za mkononi ya
 NOKIA, ambapo anatengeneza
 applications ambazo anazituma katika
 kampuni hiyo ambayo nayo bila hiana huitumia.
Hongera kwa Alvin na wazazi wake pia..

PHOTOS:Kili Music Awards(KTMA) 2013 + Yote yaliyojiri

Embedded image permalink 
Millard Ayo & Jokate
Embedded image permalink 
Host Zembwela
Watoto Wa Bibi"Jambo Squard" Kundi Bora la Mwaka
 Embedded image permalink 
Warriors From The East Best Raggae Song
 Embedded image permalink 
Amin & Linahh

Embedded image permalink 
Gardner G Habash akipokea tuzo ya msanii Bora wa Kike kwa niaba ya Lady Jaydee
Embedded image permalink 
Omy Dimpoz

Embedded image permalink 
Chaz Baba na tunzo Zake
 Embedded image permalink 
Mashujaa Band Bora ya Mwaka

Embedded image permalink 
Mtunzi Bora Wa Bongo Fleva
PERFORMANCES
 Embedded image permalink 
Amin
 Embedded image permalink
Linah Rockin 
 Embedded image permalink
Madee
 Embedded image permalink
Embedded image permalink 
Rich Mavoko
KTMA 2013 RED CARPET
Embedded image permalink 
Meneja KLM beer @KTMA red Carpet

 
Tayana, Millard Ayo na Jokate.
 
Kala Jeremiah
Embedded image permalink 
Embedded image permalink 
Embedded image permalink 
Ben Pol @The Red Carpet
Embedded image permalink 
Jose Mara
 Adam Mchomvu.
 
Maulid Kitenge, Millard Ayo na Jokate.
Millard Ayo, Brand Manger wa bia ya Kilimanjaro George Kavishe na Jokate Mwegelo.

KIKUNDI BORA CHA MZIKI WA KIZAZI KIPYA JAMBO SQUARD #KTMA 2013

Embedded image permalink

WATCH KILI MUSIC AWARDS TANZANIA (KTMA) LIVE HERE

"NATAMANI KUOLEWA NA MSANII AY".....SALAMA JABIR

 
Mtangazaji mahili wa show za TV/Radio aliyeisimamisha wima show mpya na kali inayorushwa kupitia channel 5 ‘Mkasi’ namzungumzia Salama Jabir ametupia ‘neno’ kupitia kipindi hicho kuwa huenda siku moja akaolewa na AY!

Kama uliiangalia show ya Mkasi jumatatu ama marudio yake leo (jumamosi) ambapo crew nzima ya kipindi cha mkasi chini ya C.E.O na Producer wa show Ambwene Yesaya ‘AY’ walikuwa wakieleza changamoto na mambo mbalimbali waliyokutana nayo wakati wanaanza kufanya kipindi hicho, mwishoni Salama ambae alikuwa akimuelezea AY kuwa ni msanii ambae anajivunia kufanya nae kazi kutokana na jinsi alivyomchapakazi na mtu wa kuaminika alimaliza kwa kusema “huenda ipo siku moja tutaona..!”.

Wote tunajua Salama  alivyo mtu wa utani sana, kitu kinachoongeza burudani ya ziada katika show zake, alitamka hivyo na kumgeukia AY akimuuliza, na AY mwenyewe akajikuta anacheka na kukubali.
Pengine ulikuwa ni utani tu, lakini hakuna aijuae kesho ukizingatia wote wako single!

"MNAOWANIA URAIS MSIKUBALI KUPOKEA PESA ZA HUYU MFANYABIASHARA FISADI AMBAYE NI KINARA WA MADAWA YA KULEVYA".... REGINALD MENGI


Mwenyekiti wa makampuni ya IPP Reginald Mengi ametoa ya moyoni kwa wote wenye mpango wa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania miaka miwili ijayo.


Bwana Mengi ameyatoa maombi yake ya moyoni na kuyaweka hadharani kupitia akaunti yake ya twitter June 7, na hiki ndicho alichokiandika.

“Nawaombea Mungu wanaotaka Urais wasipokee mshiko wa mfanyabiashara fisadi mkubwa ambaye pia ni kinara wa madawa ya kulevya.”

Swali ni mfanyabiashara gani, hilo linaweza kuwa ni jiwe gizani kama yupo kweli aliyetajwa litakuwa limemfikia. 
Na  kama  kuna  msomaji  wetu  anayemjua, ANARUHUSIWA  KUMTAJA  kwenye  COMMENTS  hapo  chini

MOROCCO VS TANZANIA - 2014 FIFA WCQ.

Match Kick Off @2300Hrs East African Time(EAT)
Kwa wale ambao wapo nje ya Tanzania wanaweza kuangalia mechi hii kupitia kwenye mtandao wa www.firstrow1.eu, bonyeza link hapo chini

Baby Madaha aja na nguo, perfume na viatu vyake! Avipa jina la Amore. Soma hapa

 

Mwigizaji na mwanamuziki wa mziki wa kizazi kipya baby Madaha ambaye kwa sasa yupo pande za kanda ya ziwa akifanya show maeneo mbalimbali ya mkoa huo anatarajia kuzindua brand yake aliyoipa jina la Amore ambayo itakuwa na viatu, nguo na perfume tarehe 29 mwezi huu kwenye hoteli ya Regency jijini Dar es Salaam.
 Akizungumza na bongomovies kwa simu tokea kahama, baby madaha alisema kuwa huo ni mwanzo tuu na anatarajia kufanya mengi zaidi kwa mwaka huu wa 2013.
“Kwanza nitaanza na nguo, perfume na viatu vinakuja soon, brand kama kawa ni Amore”
“Nimeamua kuingia rasmi kwenye ujasiriamali, pamoja na movie na muziki nataka nifanye na kitu kingine tofauti kidogo, mambo yanabadilika!” Huwezi jua kesho itakuaje alisema baby madaha
“Nakuja na viatu, perfume na nguo za brand ya Amore, kwa sasa vitu hivi vipo kwenye production stage ila tarehe 29 hiyo tukutane pale regency kwa uzinduzi rasmi” aliongeza madaha
SOURCE:Bongo Movies.com

HII NDO STAGE YA KILI MUSIC AWARDS(KTMA)....Kickin OFF TONIGHT

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
. 
SOURCE:Millard Ayo

CASH MONEY NI NOMA! WAMNUNULIA DRAKE BUGATI VEYRON. ICHEKI HAPA

HII NI KUTOKA KUNDI MOJA MAARUFU SANA NDANI YA PANDE ZA OBAMA, SI KUNDI JINGINE BALI NI YOUNG MONEY /  CASH MONEY. KUNDI HILI HUSIFIKA SANA KWA MEMBER WAKE KUMILIKI VITU VYA THAMANI MFANO MAGARI. NA KAMA INAVYOJULIKANA LILI WAYNE NA BIRDMAN WANAMILIKI MAGARI MENGI TU YA THAMANI. WOTE HAWA WAWILI WANAMILIKI BUGATI VEYRON. SASA BAADA YA KUKAA KAMA KUNDI WAKAONA SI VIBAYA  WAKIMNUNULIA BUGATI VEYLON DRAKE KWANI AMEKUA MCHANGO MKUBWA KATIKA KUNDI LAO. UNAWEZA ITAZAMA GARI HIYO HAPO CHINI. KWA SASA GARI HII NI MALI YA DRAKE.


HATARII...KOCHA WA TAIFA STARS KIM PAULSEN ATAKA KUMPIGA MLINZI,GETI LAFUNGULIWA KWA NGUVU HUKU MLINZI AKIBANWA KWA KUZIDIWA NGUVU NA WATANZANIA..Angalia PICHA

Kocha wa Stars, Kim Poulsen kushoto akipambana na askari wa Uwanja wa Marakech

TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars usiku huu imekiona cha moto mbele ya askari wa Uwanja wa Marakech, baada ya kufanyiwa vurugu na kuzimiwa taa ishindwe kufanya mazoezi kwenye Uwanja huo siku moja kabla ya mchezo wao na wenyeji wao Morocco kesho, kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia. 
Sheria za FIFA zinasema timu mgeni, itapewa fursa ya kufanya mazoezi katika Uwanja utakaotumika kwa mechi dhidi ya wenyeji katika muda ambao mechi itachezwa, lakini leo msafara wa Stars ulipofika Uwanja wa Marakech ulizuiwa kuingia ndani na askari wa uwanjani hapo. 
Juhudi za Kocha mkuu wa Stars, Kim Poulsen kuwaelewesha askari wa Uwanja huo sheria ili wairuhusu timu kuingia uwanjani hazikuzaa matunda na ikabidi viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) waingilie kati, nao pia wakachemsha.
Thomas Ulimwengu kulia nje ya geti, askari kushoto


Dk Dau getini

Mtanzania anaruka geti ili kufungua mlango Stars ikafanye mazoezi

Baadhi ya wachezaji wa Stars, kutoka kulia Juma Kaseja, Amri Kiemba, Mrisho Ngassa na Salum Abubakar baada ya kuingia uwanjani

Kutoka kulia Mwinyi Kazimoto, Athumani Iddi 'Chuji' na Kevin Yondan

Crescentius Magori kushoto akishuhudia marefa wa mchezo huo wakikagua pasipoti za wachezaji wa Stars

Wasiwasi; Kutoka kulia DK Dau, Mh Zitto Kabwe, Mh Mohamed Dewji na Magori wakijadiliana uwanjani

Ikawadia zamu ya viongozi wa Kamati ya Ushindi ya Stars, inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premum Lager, ambao nao walichemsha- ndipo baadhi wa Watanzania waishio hapa na wachache waliosafiri kutoka Dar es Salaam walipoongeza nguvu.
Walikwenda kufungua geti kwa nguvu, wakawaweka kando askari waliokuwa wanawazuia na kuiingiza timu uwanjani kufanya mazoezi. 
Hata hivyo, Stars ilipofika uwanjani ililazimika kusubiri tena, kwani wenyeji Simba wa Atlasi walikuwa wakiendelea na mazoezi.
Baada ya nusu saa, Morocco walimaliza awamu yao na Stars wakaanza kupasha misuli moto. Hata hivyo, baada ya dakika 34, taa za Uwanja huo zilizimwa na uwanjani kuwa giza totoro, lakini viongozi wa TFF wakaenda kuomba, zikawashwa na timu ikafanya mazoezi kwa dakika 10 zaidi. 
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Mh. Amos Makalla aliyekuwapo wakati wa vurumai zote hizo, alisikitishwa mno na kitendo hicho akisema si cha kiungwana na si cha kiunamichezo.
Makipa mazoezini; Juma Kaseja amedaka, Ally Mustafa 'Barthez' anamshuhudia kushoto


Shomary Kapombe anayeteleza, Erasto Nyoni akipitisha mpira

Mtanzania amemdhibiti askari wachezaji waingie uwanjani

Wachezaji wakiingia uwanjani kufanya mazoezi

Watanzania wamefanikiwa kufungua geti

Ahmad Mgoyi wa TFF akipambana na askari kufungua geti 

Mpambano, Kim Poulsen na askari, nyuma ni Mgoyi 

Makamu wa Rais wa TFF, Athumani Nyamlani alisema Morocco walikuja kucheza Dar es Salaam walipokewa vizuri na wakahudumiwa vizuri hadi wanaondoka, ajabu leo wanaifanyia ‘unyama’ Tanzania.
Mkuu wa Msafara wa Stars hapa, Crescentius John Magori alisema watapeleka malalamiko FIFA, waandaji wa michuano ya kufuzu kwa Kombe la Dunia na kwa kuwa ushahidi upo, anaamini Morocco watachukuliwa hatua.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe alishauri Stars icheze chini ya angalizo kwa kuwasilisha barua FIFA mapema ili wakae wanajua kuhusu hali halisi Morocco.
Kwa ujumla kilichotokea leo kimewatia woga Watanzania wengi waliopo hapa kuelekea mchezo wa kesho, ambao Stars inahitaji ushindi ili kujiimarisha katika mbio za kuelekea Brazil 2014. 
Hata ulinzi wa msafara wa Stars kutoka hotelini hadi uwanjani hakuwa wa kutosha na ilishuhuidiwa mara kadhaa ukiingiliwa na magari mengine barabarani wakati timu ikienda uwanjani kwa mazoezi.
Wenyeji nchini Morocco wanasema inapowadia mechi, huwa wanaogopa kwa sababu mara nyingi hutokea vurugu ya damu kumwagika.
Kwa ujumla Stars inaingia katika mchezo wa kesho katika hali ya wasiwasi na woga mkubwa. 
Stars itashuka dimbani saa 3:00 usiku kesho kwa saa za hapa sawa na saa 5:00 za Tanzania kucheza na Morocco.
Stars inashika nafasi ya pili katika Kundi C, ikiwa na pointi sita nyuma ya Ivory Coast yenye pointi saba, ambayo kesho itakuwa ugenini ikimenyana na Gambia katika mchezo mwingine wa kundi hilo.
Mrisho Ngassa anamiliki mpira


Thomas Ulimwengu anakwenda

Mbwana Samatta kulia na mpira

Wachezaji Stars Uwanja wa Marekch

Stars ilitua hapa Jumatatu ikitokea Ethiopia ambako iliweka kambi ya wiki moja na kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Sudan, ulioisha kwa sare ya bila mabao.
Kabla ya kuja hapa, Stars iliweka kambi ya wiki moja katika hoteli ya Tansoma, Dar es Salaam ikijifua Uwanja wa Karume na siku chache kabla ya kuondoka ilialikwa Ikulu na Rais Jakaya Kikwete, aliyewapa hamasa kwa hotuba nzuri.
credit- bin zubery