Monday, March 25, 2013

CHAMELEONE AZUNGUMZA BAADA YA KUTAJWA KATIKA ORODHA YA WANAMUZIKI 10 TAJIRI ZAIDI AFRICA

Nyota wa muziki nchini Uganda Jose Chameleone ameamua kuweka wazi juu ya suala la yeye kukubaliana au kutokubaliana na kuwekwa kwenye orodha ya wasanii nyota matajiri barani Afrika kutokana na utajiri wake alioupata kupitia muziki wake.

Hayo yamesemwea hivi karibuni kupitia jarida moja la burudani ambalo limenukuu Chameleone akisema kuwa hayupo tayari kunyanyaswa na mtu yeyote kutokana na kumiliki utajiri wake alionao kwani yeye kazi yake kubwa ni kuwapa watoto elimu yenye ubora kupitia muziki wake na sio kujigamba na kubweteka na kauli za utajiri.

Chameleone ambaye pia anatarajia kuzindua albamu yake ya nne aliyoibatiza jina Badilisha, mwezi ujao jijini Kampala amemalizia kwa kusema kuwa yeye mali si kitu kwake na utajiri mkubwa anaojivunia ni mashabiki wanaopenda kazi zake.

No comments:

Post a Comment